| Waziri ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba |
| Wakuu wa wilaya za Iringa wakiwa katika kikao cha kazi Siasa ni Kilimo |
| Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya na miji Iringa. |
| Wabunge wa Mkoa wa Iringa wakiwa katika kikao kujua hatma ya kilimo mabondeni |
| Kikao cha kazi mkoani Iringa chini ya Waziri makamba |
Waziri Ofisi ya makamu wa Rais Muungano na mazingira
January Makamba amewataka watendaji wa serikali katika halmashauri zote nchi
kutowabughudhi wananchi wanatumia kilimo cha mabondeni
maarufu kama vinyungu mpaka litakapotolewa tamuko rasmi litakalotokana na
makubaliano ya viongozi ambapo ametoa muda wa miezi mitatu kukamilisha
majadiliano yatakayolenga kutatua mkanganyiko uliopo.
Waziri makamba amesema hayo hii leo mkoani Iringa wakati alipokutana na
viongozi wa mkoa huo ili kutoa ufafanuzi juu ya suala la utunzaji wa mazingira
kwa kufuata kanuni zilizopo kutokana na sintofahamu iliyowakumba wananchi la
kuzuiwa kutumia kilimo cha mabondeni kwa lengo la kutunza vyanzo vya maji jambo
linaloifanya serikali kuwataka wananchi waendelee na shughuli za kilimo katika
maeneo waliyopo na kutoingia katika maeneo mapya.
“kumekuwa na vitendo vinavyofanywa na baadhi ya
watendaji wetu huku vijijini ambao wamekuwa wakiwakamata na kuwatesa wananchi
pale wanapowakuta wananchi wajishughulisha na kilimo huku wakitumia nafasi zao
kwa madai kwamba kuna agizo limetolewa hayo siyo maagizo leo muwambie wananchi
waendelee na shughuli zao katika maeneo waliyopo na siyo kuingia katika maeneo
ambayo bado hayajaguswa”
Katika hatua nyingine Waziri makamba ameyataka
makampuni na Taasisi zilizowekeza katika sekta ya misitu nchini kuona namna ya
kuanza kuitoa miti isiyorafiki wa mazingira katika vyanzo vya maji na kupanda
miti inayohifadhi na kutunza maji badala ya kuwatazama wananchi pekee kuwa
ndiyo sababu ya uharibifu wa mazingira.
“kumekuwa na makampuni na Taasisi ambazo zimewekeza katika
misitu na chain a zimepanda mazao hayo mpaka kwenye vyanzo vya maji tunajaribu
kuona jinsi ya kukaa nao ili waweze kuitoa kusudi wapande miti rafiki na vyanzo
vya maji badala ya kuwabana wakulima tu pekee yao ningependa ndani ya wiki tatu
tuwe na mkutano wa viongozi wote tuone namna ya kutembelea wilaya zote za mkoa
wa iringa na mabonde yote kubaini hali ilivyo huko”alisema makamba
Cosato Chumi na Venance Mwamoto ni Mbunge wa Jimbo
la Mafinga Mjini alisema wabunge richa ya kupigia kelele bungeni agizo hilo la
wananchi kutojihusisha na kilimo hicho walisema iwapo serikali isingelitazama
jambo hilo lingekuwa na athari za kiuchumi na maisha ya wananchi kwaujumla hivyo
wamewataka wananchi kuzingatia maagizo kwa kushiriki utunzaji wa mazingira kwa
vitendo.
“unapo angali athari za kimazingira ni lazima
uangalie pande zote maana usiangalie kuhifadhi mazingira wakati unaumiza wananchi
lakini inategemea na maeneo ambayo hakuna ulazima wa kufanya hivyo ukuangali
kwa wilaya mufindi na mkoa wa Iringa tayari wananchi wake wanatunza vyanzo vya
maji na kilimo cha vinyungu ni sehemu ya maisha ya wananchi kwahiyo jambo la
kuwaacha wakulima waendelee ni sawa na tunaamini watatunza zaidi vyanzo vya
maji”alisema Chumi
Venance Mwamoto ni Mbunge wa Jimbo la Kilolo kwa
upande wake alisema changamoto iliyopo ni pamoja na kukosekana kwa elimu ya
utofautishaji wa neon chanzo cha maji serikali iliona vyema kupiga marufuku
lakini najua mkoa wa iringa unaasilimi zaidi ya 70% ya wananchi wake
wanategemea kilimo cha vinyungu tayari tungeanza kuona madhara kwenye masoko
kukosekana kwa Mboga halmashauri zingeanza kukosa mapato kwahiyo tunashukuru
kwa uamuzi huu unatupa nguvu ya kufanya ziara kwenye majimbo yetu”alisema
Mwamoto
Kwa upande wao baadhi ya Madiwani wamepongeza
jitihada zilizofanywa na serikali kwani wanasema kuzuiliwa kwa kilimo cha
mabondeni kulikuwa na Athari za moja kwa moja kwa wananchi kwani wananchi kwa
kiasi kikubwa wanategemea kilimo hicho kutokana na msimu wa mvua kuwa mmoja
Hivi karibuni Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano
wa Tanzania Samia Suruhu Hasan aliunda kikosi kazi ili kufanya upembuzi juu ya
kulinda na kuokoa mto ruaha mkuu unaoonekana kuathiriwa na shughuli za kijamii
huku mkoa wa iringa ukitegemea kilimo cha mabondeni ili kuwatoshereza wananchi
kupata kipato na chakula.
leo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni