- Acheni kuwatisha wananchi kuweni na Unyenyekevu
- Suala la kodi katika mashirika ya Dini kikwazo na mzigo kwa uendeshaji wa huduma
- Serikali iendelee kuwatumikia wananchi kwa misingi ya sheria
![]() |
| Askofu Dkt Fredlick Shoo Mkuu wa Kanisa KKKT |
![]() |
| Askofu wa Dayosisi ya Iringa Braston Gavile(kulia)na Msaidizi wa Askofu Hamidu Saga(kushoto) |
![]() |
| Maaskofu waliohudhuria Ibada ya Kuwekwa wakfu Askofu mpya Dayosisi ya Iringa Mch Braston Gavile |
| Jamuhuri Wiliumu Mkuu wa Wlaya ya Mufindi akimwakilisha mkuu wa mkoa wa Iringa |
Viongozi wa Dini na
Serikali nchini wametakiwa kuwa na uzalendo katika kutekeleza majukumu yao kwa
kuwatumikia wananchi bila kuwabagua wala kutangukiza masilahi yao jambo
linaloweza kuwagawa watanzania.
Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili La
Kilutheri Tanzania Askofu Dkt Fredrick Shoo wakati wa ibada ya kumumweka wakfu
na kumuingiza kazini Askofu Mpya wa Dayosisi
ya Iringa ambapo amesema ni vema kila kiongozi akatumia madaraka yake kwa
kuwatumikia wananchi badala ya kutumia vitisho na kutumia mamlaka yao vibaya
jambo linaloshusha heshima kwa viongozi kutokana na matendo yao.
“ndugu zangu viongozi wa kiroho na seriakli mliopo hapa
tumepewa mamlaka kuwaongoza watanzania siyo kwa kuwatisha bali ni kwa
unyeyekavu ili tuwasaidie watambue uhuru wao heshima ya kiongozi yeyote itakuja
kwajinsi ulivyowatimikia watu wa Mungu,Mungu amekupa nafasi hiyo ili uwatumikie
watanzania ili tuiinue nchi yetu taifa letu lisonge mbele kimaendeleo”alisema
Askofu Shoo
Aidha Mkuu huyo wa Kanisa hakusita kuwanyoshea kidole baadhi
ya viongozi wanaotumia nafasi zao kwa kujinufaisha wenyewe badla ya kujali masilahi mapana ya nchi na
kuendelea kuona wao ni zaidi kuliko watu wengine hivyo amewataka viongozi wa
serikali na Dini nchini kuwa na uzalendo na nchi yao.
“yapo mambo ya aibu yaliyofanywa na baadhi ya viongozi
waliolitumikia Taifa hili badala ya
kufanyakazi ili watu wote wanufaike unakaa kusaini mkataba ambao unaiumiza nchi
yako unajiita umesoma hebu tuipende nchi yetu badala ya kuuza nchi kwa masilahi
binafsi na kuingia mikataba na mabeberu wa nje.”alisisitiza Shoo
Akizungumza mara baada ya kusimikwa kuwa Askofu Mkuu wa
Dayosisi ya Iringa Mch Braston Gavile richa ya kupongeza kazi inayofanywa na
serikali ya awamu ya Tano hakusita kuzungumzia kilio cha Taasisi za dini
kutokana na tozo la Kodi katika huduma wanazozitoa ikiwemo Afya na Shule kuwa
zimekuwa zikitozwa kodi kubwa bila kutambua taasisi hizo hazifanyi biashara bali zinatoa huduma.
“taasisi za dini zinashindwa kuendelea kutoa huduma kutokana
na kodi zimezidi ikumbukwe kuwa taasisi hizi hazifanyi biashara bali zinatoa
huduma tunaomba seriakali yetu iangalie kwa upya suala la kodi nchini kwa mashirika ya Dini kwamaana kodi hizo
zimekuwa mzigo mkubwa katika uendehaji wa huduma hizo”alisema Askofu Gavile
Jamuhuri Wilium ni mkuu wa wilaya ya Mufindi akizungumza kwa
niaba ya mkuu wa mkoa wa Iringa amesema serikali inayoimani kubwa kwa makanisa
kwa kazi ya kutoa mafundisho na kukemea maovu jambo linalofanya kuongeza
ushirikiano baina ya mihimili hiyo miwili ambapo ametumia nafasi hiyo kuwataka
viongozi wa Dini kuendelea kumuombea Rais wa Jamuhuri ya Tanzania ili aendelee kuwatumikia
watanzania na kutetea rasilimali za nchi,
“serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi za Dini kwani
tunatambua mchango mkubwa unaotolewa na Taasisi hizi tunakupongeza Baba Askofu
kwa kuaminiwa na leo unaanza kuwatumikia wananchi rasmi mimi niseme tuiunge
mkono serikali na tuiombee ifanye vizuri katika kuwaletea wananchi maendeleo ya
kweli.”alisema mkuu wa wilaya
Kanisa la Kiinjili Tanzania ni miongoni mwa makanisa yenye
waumini wengi ambapo kwasasa lina jumla ya waumini zaidi ya million 6.7 ambapo
wameaswa kuendelea kujituma kufanya kazi ili kujiletea maendeleo na Taifa kwa
ujumla.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni