![]() |
| Asiah Abdallah Mkuu wa Wilaya ya Kilolo |
![]() |
| Bi Amina Masenza mkuu wa Mkoa wa Iringa akizungumza na umati wa watu walialikwa katika Futari |
![]() |
| Richard Kasesela mkuu wa Wilaya ya Iringa |
![]() |
| Jamuhuri Wilium Mkuu wa Wilaya ya Mufindi |
![]() |
| Baadhi ya waalikwa katika Futari ya Mkuu wa Wilaya Kilolo |
Waumini wa Dini ya Kiislamu nchini wamemetakiwa
kudumisha umoja na mshikamano miongoni mwa jamii ikiwa ni pamoja na
kushirikiana na serikali katika kuliletea Taifa maendeleo.
Akizungumza katika Hafla ya futari iliyoandaliwa na
mkuu wa wilaya ya Kilolo mkuu wa mkoa wa iringa Amina Masenza alisema katika
baadhi ya maeneo kumeibuka Tabia ya baadhi ya watu kutumia kigezo cha Dini
kufanya vitendo viovu ikiwemo utapeli jambo linalolenga kuchafua Uislamu huku
akitumia nafasi hiyo kutoa wito kuiunga mkono serikali katika kuhakikisha
inawaletea maendeleo ya kweli wananchi.
“niwaombe ndugu zangu waislamu tunapowaona watu
tunaowatilia mashaka wanakuja katika maeneo yetu ya Ibada wakijifanya waislamu
kumbe wanamambo yao wanafanya hebu tutoe taarifa kwa vyombo vinavyohusika kwani
uislamu utalindwa na waislamu wenyewe lakini pia ndugu zangu niwaombe
tushirikiane na serikali katika kujiletea maendeleo”alisema mkuu huyo wa mkoa
Aidha katika hatua nyingine Masenza alitoa wito kwa
wananchi kutunza chakula hususani katika msimu huu wa mavuno ambapo mara nyingi
baadhi ya wananchi hutumia mazao yao kwa pupa na mwishowe hujikuta wameishiwa
kabisa hivyo alisema ni vyema wananchi wakahifadhi chakula bila kusahau
utunzaji wa mazingira hususani vyanzo vya maji kwa manufaa ya vizazi vijavyo.
“nitoe wito kwa wananchi wote waone umuhimu wa
kutunza chakula kwani tusipofanya hivyo tatizo la njaa litatumaliza wapo wenye tamaa
ya fedha wanauza mazao yao bila kuweka akiba niwaase tunzeni chakula chakutosha
kwaajili ya familia zenu lakini pia mkumbuke utunzaji wa mazingira hasa katika
vyanzo vya maji ni muhimu kwasasa na baadae mazingira ni uhai”alisema Masenza
Kwa upande wake mkuu wa wilaya Kilolo Asiah Abdallah
akizungumza wakati akiwakaribisha wageni waliohudhuria hafla hiyo ya Futari
hakusita kuwakumbusha watanzaniani kuwa nchi hii imepata Rais ambaye Mungu
amemchagua jambo la msingi ni kumuunga mkono kwa kazi zake anazofanya maana
wapo wanaombeza hivyo aliwataka watanzania kuwapuuza watu hao.
“kila analolipanga mungu lazima litimie Mwenyezi
Mungu alipanga Tanzania kuanzia mwaka 2015/2020 tuwe na Rais shupavu John Pombe
Magufuli na imekuwa hatuna budi kumuunga mkono kwa yote anayoyafanya kwa
masilahi ya watanzania wote “alisema mkuu huyo wa wilaya
Naye Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jumuhuri Willium
richa ya kuwataka wananchi na waumini wa Dini ya Kiislamu kutumia vyema mwezi
huu Mtukufu wa Ramadhani aliitaka jamii ijikite katika kuombea amani na umoja wa
nchi yetu hata mara baada ya kumaliza
mufungo huo.
“ningependa sana tuutumie mwezi huu wa Ramadhani
katika kujitafakari na kumurudia muumba wetu maana kwake ndiko tunakopata Amani
tudumishe amani na upendo miongoni mwetu na jamii inayotuzunguka”alisema
Jamuhuri
Lakini pia mkuu wa wialaya ya Iringa Richard
Kasesela ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria hafula hiyo ambaye aliwataka
waumini wa Dini ya Kiisilamu kutumia uislamu kwa kufanya matendo yanayompendeza
Mungu kwani wapo wanaoamini kuwa na alama katika Paji la Uso ndiyo kipimo cha
ukamilifu wake bali ni vile wanavyoenda.
Awali wakizungumza katika hafla hiyo Mashekhe wa
Mkoa na Wilaya ya Kilolo Abubakari Chalamila na wameitaka seriakali
kuwashirikisha katika utoaji wa matamko kwani ipo tofauti pindi tamko
linapotolewa na Kiongozi wa Dini jamii huelewa zaidi kuliko linapotolewa na
kiongozi wa kisiasa.
“kauli za viongozi wa Dini husikilizwa na huaminiwa
zaidi kuliko kauli za wanasiasa tutumieni kwa kuwa yote yanayopigiwa kelele na
serikali hii yapo katika vitabu vya mungu nasi tunao wajibu wa kukemea na
kuonya pale mtu anapofanya kinyume na agizo la Mwenyezi Mungu hivyo
tushirikiane kuijenga nchi yetu”walisema mashekhe
Ilielezwa kuwa miongoni mwa matendo yanayochochea
umoja na Mshikamano miongoni mwa jamii ni pamoja kukaa pamoja kila mmoja
akitafakari namna anavyoweza kulinda na kusimamia amani iliyopo kwani hiyo
ndiyo njia pekee ya kuwaunganisha watanzania.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni