Jumanne, 23 Desemba 2014

Vocaroo Voice Message

Mwimbaji wa Nyimbo za Injiri Nyanda za juu kusini anayetarajia kuanza rasmi show mbalimbali na mona kati ya vibao alivyonavyo ni hiki kinasema ANAWEZA

Ijumaa, 5 Desemba 2014

Mwasabwite kukonga Tamasha la Krismasi

 index

Na Mwandishi Wetu MWIMBAJI wa nyimbo za injili nchini Edson Mwasabwite anayetamba kwa sasa na kibao chake kijulikanacho kwa jina la ‘Ni kwa Neema na Rehema’ amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika Tamasha la Krismasi litakalofanyika katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Songea Desemba mwaka huu. Mwasabwite alisema amejipanga kikamilifu kukonga nyoyo za mashabiki wake katika tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Desemba 25, 26 na 28 hivyo mashabiki zake wajitokeze kwa wingi kupata burudani ya nguvu kutoka kwake. Mwasabwite alisema mwaka huu watanzania wakae mkao wa kula kwa kusifu na kuabudu katika Tamasha la Krismasi kwani tayari amezindua albamu yake ya pili ijulikanayo kwa jina la ‘Asilimia mia Mungu amenihurumia’ yenye nyimbo tisa. “Nimejipanga vizuri kutoa burudani kwa mashabiki wangu katika tamasha la mwaka huu la Krismasi kwani maandalizi ni mazuri, safari hii itakuwa zaidi ya mwaka jana kwa sasa nina nyimbo nyingi zitakazowabariki mashabiki zangu na tayari nimeshazindua albamu mpya,” alisema Mwasabwite. Aidha amempongeza Mkurugenzi wa Msama Promotions kwa kuweza kuandaa Tamasha kubwa la Kikristo lenye mafanikio makubwa kwa kuweza kuwakutanisha waimbaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania kwa lengo la kutangaza injili Tanzania. “Makampuni ya Msama yanaaminika na kukubalika kwa watanzania na nchi nyingine za jirani ndio maana hata tamasha linafanikiwa, tunaomba wananchi waendelee kununua kazi zetu, tunaomba sapoti kutoka kwa waumini na mashabiki wa muziki wa Injili,” alisema Mwasabwite.

 

MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA KUJITOLEA DUNIANI

Siku ya Kimataifa ya Kujitolea Duniani huadhimishwa tarehe 5 Desemba kila mwaka kwa lengo la kutambua mchango wa kujitolea unaotolewa kwa ajili ya maendeleo katika jamii tunamoishi, kitaifa na kimataifa.
Kujitolea hujumuisha hiari, umoja, utu na kuaminiana na kunatoa fursa muhimu katika kupambana na maradhi, ujinga, umasikini, hifadhi ya mazingira na maeneo mengi ya kimaendeleo ambayo yanahitaji msukumo.

Aidha, kujitolea kunatoa mchango muhimu katika kushughulikia majanga pale yanapotokea, kuimarisha umoja katika jamii na kuboresha maisha ya watu.

Tanzania kama sehemu ya jamii ya Kimataifa itaadhimisha siku hiyo katika katika ukumbi wa Chuo cha Utalii kilichopo karibu na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM),saa mbili na nusu asubuhi.
Kaulimbiu ya Maadhimisho hayo mwaka huu ni ‘Ushiriki na Ushirikishwaji katika kuleta maendeleo  katika ngazi zote za mitaa, taifa na kimataifa.’

Katika maadhimisho hayo, wananchi hasa vijana watashiriki katika mdahalo kuhusu umuhimu wa kujitolea kwa ajili ya kuleta maendeleo. Aidha, kutakuwa na shuhuda na maonyesho ya taasisi zinazoshiriki katika shughuli za kujitolea ili kuhamasisha na kufufua moyo wa kujitolea miongoni mwa jamii.

Watanzania hususan Vijana wanahamasishwa kuibua shughuli za kujitolea na kushiriki katika zile zilizokwisha anzishwa  ikizingatiwa kuwa wao ndiyo nguvu kazi kubwa ya jamii.

Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo inawakaribisha wananchi wote kushiriki katika maadhimisho hayo muhimu ili kushiriki katika mdahalo huo na kujionea jinsi watu mbalimbali wanavyotoa mchango mkubwa katik jamii kupitia shughuli za kujitolea.
Top of Form
Bottom of Form
Bottom of Form

 

Jumatano, 12 Novemba 2014



MUCOBA BENKI YAWA CHACHU YA MAENDELEO KWA WAKULIMA MKOANI IRINGA

Meneja wa Benki ya Wananchi MUCOBA Bw Beny Mahenge akielezea utendaji wa Benki hiyo
Wadau wa Benki ya wananchi MUCOBA
Wakulima wa mkoa wa Iringa wameanza kunufaika na ruzuku za pembejeo kupitia Benki ya wananchi Mufindi(MUCOBA) ambayo kwa sasa inajulikana kwa jina la MUCOBA Bank PLC ikijumuisha wananchi wote wa mkoani wa Iringa imeanza kutoa mikopo ya pembejeo kwa vikudi vya wakulima.

Akielezea juu ya namna mwananchi atakavyonufaika na ruzuku hiyo Meneja wa Benki hiyo Bw Ben Mahenge amesema serikali imeamua kutoa ruzuku kwa mkulima kupitia Benki ya wananchi kutokana na ukaribu wa Benki hiyo kwa wananchi wa maeneo yote ya mkoa wa Iringa ili kulinda usalama wa chakula kwa mkulima.

Amesema kuwa walengwa wakuu ni wananchi wa kipato cha chini ili wawe na uhakika wa kupata chakula cha kutosha hususani kwa wale waliolima ukubwa wa shamba la kuanzia ekali moja ambao watasaidiwa kupatiwa ruzuku ya mifuko mitatu ya mbolea na mfuko mmoja wa mbegu kwa mazao ya Mpunga na Mahindi ikiwa ndiyo mazao pekee yanayopendelewa na wananchi wa mkoa wa Iringa.

Bw Mahenge ameendelea kufafanua juu ya ruzuku hizo kuwa itatolewa kwa wakulima watakaojiunga katika vikundi mbalimbali vitakavyojumuisha wanakikundi wasiopungua 10 ambao kila mmoja atapatiwa mkopo wa pembejeo zenye ruzuku ya serikali.

Ameelezea kuwa ruzuku hiyo itatokana na riba ya mkopo atakaoupa kutoka benki ambayo ghalama yake ya ni 18% ambapo serikali inalipa riba ya asilimia 14% ya riba ikiwa kwa upande wa mkulima atalipa riba ya asilimia 4% kutoka kwenye riba ya asilimia 18% ya mkopo wote.

Aidha amesema kupitia benki hiyo ya MUCOBA wananchi watajipatia pembejeo wanazozihitaji badala ya kupangiwa aina ya pembejeo za kilimo ili kuboresha zaidi kipato na mazao ya mkulima ambapo amesema mkopo huo utalipwa baada ya mavuno pamoja na kwa kabla ya mkulima kupewa mkopo huo atatakiwa kulipa asilimia 20 ya kianzio kuonesha nia ya kuhitaji ruzuku.

Hivyo amewataka wananchi kushiriki katika vikundi mbalimbali ili wawe sehemu rahisi ya kupata pembejeo zenye ruzuku ya serikali kwa urahisi zaidi pia amewataka wakulima kumchangua wakala wa pembejeo atakayeshirikiana katika kuzipata zenye viwango vya hali ya juu.

Jumanne, 11 Novemba 2014


HATARI!! Diamond aamua kuwapa ''makavu live'' team Wema baada ya wao kumdiss.

HATARI!! Diamond aamua kuwapa ''makavu live'' team Wema baada ya wao kumdiss.

Baada ya mashabiki wa mwanadada Wema "kumjia juu mwanamuziki Diamond Platnumz" kuhusu tuhuma za yeye kumtumia mwanadada huyu kimwili zaidi bila kumuendeleza, hatimaye raisi huyu wa kundi la WCB ameamua nay eye kufunguka haya mazito juu ya kauli hizo. Kupitia ukurasa wake wa mtandao ule maarufu wa kijamii Diamond ameandika haya..

“Nafkiri ningewaona kweli Mnaakili na Mapenzi ya dhati kwa Msanii wenu... kama mngemshauri apunguze Mashoga wapenda anasa na apunguze Stareh zisizo na Faida, wenda ingemsaidia Pesa kuzitumia kwenye kufanya kazi na kuleta maendeleo badala ya kuwapa viwanda vya pombe...
Mimi kama bwana, wajibu wangu ni kuhakikisha Mpenzi wangu anakula vizuri, anavaa vizuri, analala vizuri, na kumuwezesha mtaji wa kufanyia kazi. Waswahili wanasema Mchungaji bora anatakiwa kuhakikisha anampeleka Ng'ombe wake Kwenye Maji safi....ila yeye ng'ombe mwenyewe ndio anatakiwa aamue kunywa maji!!!!! Au mnataka nikishampa mtaji niache kufanya na show tena na kuigiza nimuigizie mie ???? Nisiende Studio nikae dukani nimuuzie mie????.. ni juhudi zako kwanza!... leo hii mimi Hata ningepewa Mamilioni ya mamilioni kama nisingekuwa na moyo wa mie mwenyewe kwanza kutaka kujituma na kupenda kufanya kazi yangu nisingefikia hapa nilipo!....Mxieeeeeeeew!


MADIWANI MANISPAA YA IRINGA WAANZA KUTAKELEZA KAULI YA KATIBU MKUU WA CCM KWA VITENDO.

Baraza la Madiwani manispaa ya Iringa lakumbushwa umuhim wao katika kusimamia miradi ya Maendeleo ikiwa ni nguzo ya muhim katika kuendeleza uchumi wa familia,jamii na Taifa.

Hayo yamejili mwisho wa wiki katika kikao charobo ya mwaka wa fedha 2014/2015 cha  Baraza la Madiwani wa halmashauri ya Manispaa ya Iringa mjini ambapo Meya ambaye pia ndiye alikuwa mwenyekiti wa baraza hilo Aman Mwamwindi aliwambia madiwani kuwa nisehemu ya serikali hivyo wanaowajibu wa kusimamia miradi inayoanzishwa na serikali ikiwemo miradi ya Afya,elimu,miundombinu na shughuli za uchumi ili kuongeza upatikanaji na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
 
Alisema pamoja na kwamba madiwani hao wanashiriki kwa kiasi kikubwa katika usimamizi wa miradi hiyo lakini pia alipata fulsa ya kuwakumbusha kuwa usimamizi wa miradi hiyo unashirikisha viongozi wa ngazi ya kijiji hadi Taifa,wananchi wa maeneo husika pamoja na asasi za kiraia na kashirika yasiyo ya kiserikali ikiwa na lengo la kuboresha maisha ya watanzani.

“Waheshimiwa madiwani tumekuwa mstari wa mbele kusimamia miradi inayoanzishwa katika kata zetu japo wapo wachache ambao kazi yao ni kuturudisha nyuma kwa makusudi maana tumekuwa na miradi mingi na inafanya vizuri kwaajili yetu sote na jamii zinazotuzunguka sasa unapoona mtu anaingiza kitu ambacho kinarudisha nyuma juhudi za serikali ukanyamaza manaake unashiriki mojakwamoja kuangamiza maisha ya watanzani”alisema meya

Hivyo amesema usimamizi mbovu wa miradi ya maendeleo mara nyingi inasababisha baadhi ya miradi kufanyika chini ya kiwango.
Baraza hilo pia lilipata nafasi ya kupata semina juu ya ushiriki wao katika mapambano dhidi ya rushwa ambalo limekuwa janga la dunia ambalo limekuwa likiwahusisha zaidi watendaji wa serikali.

Akitoa semina hiyo Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU)Bw Ismail Bukuku aliwambia madiwani kuwa lengo la semina hiyo ni kuwakumbusha uwajibikaji kwa kufuatamisingi ya sheria huku wakitambua usimamizi mzuri wa raslimali za umma kutasaidia kuziba mianya ya Rushwa,itasaidia fedha za miradi kutumika kwa malengo yaliyo kusudiwa.

Huku akiwataka madiwani hao kuwaelimisha wananchi kutambua haki zao katika kupata huduma za msingi ikiwa nipamoja na matibabu,ajira,elimu bila kutoa wala kupokea rushwa vilevile  kuzijua sheria.

Jumatano, 22 Oktoba 2014

TUKIWA NA WATU KAMA HAWA HAPA KWETU TUNAIMANI AMANI IPO BILA SHAKA.





Jumatano, 24 Septemba 2014



 MH.MGIMWA AWAHAMASISHA VIJANA KUUNDA VIKUNDI ILI WAWEZESHWE.
Mh.Gogfrey Mgimwa Mbunge wa Jimbo la Kalenga
Vijana nchini wametakiwa kujiunga katika vikundi vya ujasiliamali vitakavyo warahisishia kupewa dhamana ya mitaji kutoka katika mifuko ya vijana ya serikali.

Rai hiyo imetolewa na Mbunge wa Jimbo la Kalenga mkoani hapa Mh.Godfrey Mgimwa wakati wa mahojiano maalumu na Overcomers redio katika kipindi cha tujadili asubuhi kuhusu namna viongozi wanakusudia kuwapa fulsa vijana wote pasipo kuangalia mjini wala vijijini.

Mh.Mgimwa amesema imefika wakati wao kama viongozi vijana kupigania maslahi ya vijana na haki zao za kuwezeshwa kimaisha ili waweze kujikwamua kiuchumi kwani kwa kufanya hivyo fedha za mifuko ya vijana zitawafikia katika vikundi.

Hivyo amewataka vijana kushirikiana kwa pamoja katika kujiletea maendeleo.