![]() |
| DC Richard Kasesela Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya Ya Iringa |
| Gloria Mnyonge Muuguzi wa zamu Hospitali ya Rufaa Iringa. |
![]() |
| Msungu Shija Mchimbaji wa madini Nyakavangala |
![]() |
| Wachimbaji wa madini wakiwa kazini Eneo la Nyakabangala Wilaya ya Iringa |
Watu 9 ambao niwajimbaji
wa madini katika mgodi wa nyakavangala uliopo katika tarafa ya ismani mkoani iringa
wamenusurika kufa kwa kuvamiwa na watu wanaosadikiwa ni majambazi huku watu wawili
wakiwa katika uangalizi wa madaktari ambapo majambazi hayo yakifanikiwa kupora pesa
zaidi ya shilingi milioni 81 pamoja na gram 400 za dhahabu.
Sayari ya Habari ilifanikiwa
kuzungumza na baadhi ya Majeruhi Msungu Shija mkazi wa Geita,Eliasi Mushi mkazi
wa Arusha ambao wanasema baadaya kuteswa kwa muda mrefu ndipo bosi wao akajitokeza
na kupigwa nyundo za miguu huku wakidai kuwa walikuwa wakimtafuta kwa zaidi ya
wiki mbili bila mafanikio na wakihitaji madini pamoja na fedha.
“Ilikuwa majira ya saa moja jioni wakaja watu 8 wakatuambia tupo chini ya ulinzi tukalala
chini wakaanza kupiga na nyundo wakasema wanamtaka bosi tukauliza shida nini
hawakusema wakamfuata ndani walipomkuta wakamtoa nje huku wakimpiga wakitaka
atoe hela za madini yaliyopatikana juzi ikabidi atoe wakaondoka lakini
kwasababu pale hakuna kituo cha polisi ilikuwa shida kupata msaada
walitusurubisha kwa muda kama wa saa moja ”.
Gaspa mbanda nimiongoni
mwa wachimbaji wadogo ambaye aliyenusurika anasema baada ya kusikia milio ya risasi
alijificha alisema wakati majambazi hao wanavamia baadhi ya wachimbaji walikuwa
bado wapo mgodini akiwa katika harakati za kutoka mgodini ndipo aliposikia
milio ya risasi akamrazimu ajifiche ili kunusuru maisha yake jambo lililomfanya
kuiomba serikali kujenga kituo cha polisi ili kimarisha hali ya ulinzi nausalama
kwa wachimbaji hao kwani katika eneo hilo hakuna kituo cha polisi.
“nilikuta watu wakipiga
kelele kudai kuwa wamevamiwa tena alikuwa ndugu yangu ambaye alikuwa ameuza
mzigo kutazama nikakuta amekamatwa na anapigwa walipoondoka majambazi hao
ilibidi tuwachukue kuwaleta hospitali kwa kweli hakuwa tukio zuri maana tupo
zaidi ya watu 3000 katika hili eneo kama ingewezekana serikali itujengee kituo
cha polisi pale tunaomba ili usalama uwepo”.
Kwaupande wake muuguzi wazamu
katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa Grolia Mnyonge alikiri kupokea baadhi
ya majeruhi ambao kwasasa wanaendelea kupatiwa matibabu na wanne wanendelea vizuri
na huku wawili wakiwa katika hali mbaya.
“Hapa tumepata majeruhi
wanne mmoja ameruhusiwa wamebaki watatu mmoja yupo chumba cha Upasuaji ambaye
hali yake bado si nzuri baadhi yao wana michubuko midogomidogo miguuni na
mikononi hali zao zikiendelea kuwa hivi watakuwa vizuri pasipo shaka”.
Akizungumzia tukia hilo
mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Iringa ambaye ndiye mkuu wa
wilaya ya iringa Richard kasesela amwaambia wandishi wa habari kuwa takribani
wiki sita kumekuwa na ongezeko kubwala watu wanaokwenda kutafuta riziki
kutokana na kupatikana dhahabu lakini jana kunatukio la uvamizi limetokea majambazi
waliokuwa na silaha mbalimbali za jadi ambapo aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni
Mginya Dadae mkazi wa Morogoro (38),Bakari Beka,Sungali Shija mkazi wa Geita,Fadhiri
Ramadhan,Nsulwa Msanda,Odrick Michael,Kitandu Mabura,Daniel Msonja,Elia Mushi,na
aliwataka wachimbaji hao kuacha tabia kutembea na fedha nyingi hali itakayo saidia
kupunguza matukio ya ujambazi .
“ni kweli tukio hilo
limetokea katika wilaya yetu lakini Jeshi la polisi linaendelea na upelelezi
kuwasaka wahusika wa kosa hilo lakini niwaombe wananchi na wachimbaji kutumia
njia mbadala katika kulipana fadha badala ya kutembea na fedha mkononi”.
Tangu kugundulika uwepo
wa madini katika kijiji cha nyakavangala tarafa ya isimani kumekuwanaongezeko
la watu kila uchwao kutoka mikoa mbalimbali nchini ambapo mpaka hivi sasa eneo hilo
linatajwa kuwa na zaidi ya watu 5000.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni