Jumatatu, 12 Juni 2017

JESHI LA POLISI MKOANI IRINGA LINAWASHIKIRIA WATU 7 KWA TUHUMA ZA KUHUSIKA NA KUVAMIA NA KUJERUHI WACHIMBAJI WA MADINI KATIKA MGODI WA NYAKAVANGALA

RPC JULIUS MJENGI AKIONESHA SILAHA ILIYOKAMATWA WAKATI WA MSAKO 

Jeshi la polisi mkoani Iringa linawashikiria watu 7 kwa tuhuma za kushiriki katika tukio la kuvamia na kujeruhi wachimbaji wadogo wa madini katika mgodi wa Nyakavangala uliopo Tarafa ya Ismani na kupora fedha pamoja na Dhahabu Gram 400.

Akitoa Taarifa kwa wandishi wa Habari juu ya kushikiriwa kwa watuhumiwa hao Kamanda wa Polisi Mkoani iringa Julius Mjengi amesema mara baada ya kupokea taarifa hizo jeshi la polisi limefanya msako kuwatafuta watuhumia ambapo hadi sasa tayari wamefanikiwa kuwashikiria watu 7 wakiwa na silaha 1 aina ya Bastola inayodaiwa kutumika katika uvamizi huo kama anavyoeleza.

kufuatia tukio lililotokea mnamo 09/06/2017 majira ya saa moja na nusu usiku katika machimbo ya nyakavangala majambazi 9 yaliwavamia wachimbaji wadogowadogo na kuwalazimisha walale chini na kuanza kuwashambulia kwa nyundo na nondo ambapo katika tukio hilo watu 9 walijeruhiwa na mpaka sasa watu 7 tunawashikiria na tunaendelea kuwa hoji ambapo wawili baadhi yao tumewakuta na silaha Bastola kwani walikuwepo kule katika eneo la tukio kwahiyo tunaendelea kuwahoji na upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani”alisema kamanda Mjengi
 
jana majira ya tatu usiku shimo moja wapo la wachimbaji wadogo wa madini lilititia na watu nne walifunikwa lakini tayari watatu wameokolewa lakini mmoja bado anatafuta katika shimo lile hivyo mpaka sasa bado hatujapata taarifa yoyote hivyo tutawajulisha pindi atakapo patikana”alisema kamanda Mjenga

Richa ya jeshi la polisi kufanya doria katika maeneo hayo bado changamoto kubwa inayotajwa ni uhaba wa mawasiliano yanayochangia kwa kiasi kikubwa ucheleweshaji wa taarifa pindi kunapotokea tatizo ambapo wito umetolewa kwa serikali kuboresha mawasiliano katika eneo hilo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni