Jumanne, 20 Juni 2017

TATIZO LA KUKOSEKANA KWA SOKO LA VITUNGUU WAKULIMA WATELEKEZA MASHAMBA YAO IRINGA



Wakulima  wakipembua na kuundaa vitunguu ili kutafuta wateja      


Idhaa Ally ni miongoni mwa wakulima wa vitunguu katika neneo hilo alisema kuwa kutokana na changamoto hizo wakulima wengi wameathirika kiuchumi na kisaikolojia kutokana na wakulima wengi kukopa fedha benki kwa ajili ya kilimo lakini mwisho wake wameambulia patupu.
“kilimo cha vitunguu kinatumia gharama kubwa kuanzia kuandaa shamba na matunzo ya mazao lakini ukija kwenye mavunohatupati faida ila changamoto inakuja kwenye soko na ukiangalia wengi wetu wakulima tumechukua mikopo na mikopo hiyo tunashindwa kurudisha kutokana na mazao kutonunulika.”alisema Ally.
Naye Chacha Omary alisema kuwa pembejeo za kilimo zimekuwa gharama kubwa sana kiasi cha wakulima wadogo kushindwa kumudu gharama hzo na aliiomba serikali kupunguza gharama za pembejeo za kilimo ili wakulima wadogo waweze kumudu gharama za pemebejeo hizo.
Kwa upande wake Elizabeth Chilala ambaye amelima hekari mbili alisema kuwa ametumia zaidi ya Mil.4.5 lakini ameambulia kupata magunia 70  tu hali ambayo imemkatisha tamaa ya kuendelea kulima zao hilo kutokana na gharama za uendeshaji kuwa kubwa.
“Hapa nimelima hekari mbili,nimetumia Mil.4.5 na nimepata gunia 70 licha ya kwamba kanuni zote za kilimo nimefuata,na kukokana na kukosekana kwa masoko ya uhakika vitunguu vyangu vitaozea shambani.”alisema Chilala
Chilala alisema kuwa matarajio yake alikuwa auze gunia moja kwa sh.100,000 hadi 150,000 lakini hali imekuwa tofauti na kulazimika kuuza kwa gunia moja 50,000.
Naye ofisa kilimo wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Lucy Nyalu alikiri changamoto hiyo na kusema wao kama serikali wanawahamasisha wakulima kulima kilimo cha kibiashara ili kujihakikishia kuwa na kipato pamoja na chakula cha uhakika.
Kuhusu masoko alisema kuwa wakulima wengi wanapoona fursa kwenye kitunguu wengi wao wanakimbilia kulima zao hilo badala ya wachache kulima na wengine kuendelea kulima mazao mengine hali inayowasababishia kwa sasa kulima kulima kwa wingi na kukosa masoko.
Nyalu alisema wao kwa sasa wanahamasisha wakulima kulima kilimo cha mkataba ambacho wanahamasisha kupitia (SAGCOT).
“Mtu azalishe pale anapokuwa ana mtu wa kununua hivyo ukipata mnunuzi anakuambia niletee tani kadhaa lakini kwa sasa hali imekuwa tofauti mazao yamekuwa mengi sokoni,bei imepungua kutokana na gharama alizotumia kuzalisha.”alisema Nyalu.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Vijijini Robert Masunya alisema kuwa halmashauri inatambua masuala ya lumbesa na pia inatambua sheria ya wakala wa vipimo ya mwaka 2002 sura ya 340 ambayo inatoa mwelekeo mzima juu ya usimamizi wa mazao kwa kuzingatia uzito.
“Kwa mfano mahindi ujazo usizidi Kilo 90,nyanya kwa teka kilo 50,vitunguu kilo 70 na mchele kilo 100 na magunia mengi yanaweza yakaeleweka kama ni lumbesa ama sio lumbesa na kama magunia yamezidi ujazo huo maana yake ni lumbesa na wajibu wa serikali ni kusimamia sharia hiyo na kuwataka wakulima wasiuze kwa uzito ambao unazidi hivyo vipimo.”alisema Masunya.
Masunya alisema licha ya kutoa sheria hizo kwa  wananchi na viongozi wa vijiji kuwataka wasimamie lakini tatizo linakuja kwa wanunuaji ambao wanawalazimisha wakulima kuuza kwa bei wanayotaka pamoja na lumbesa na hivyo suluhisho ni taasisi na wadau wote kushikamana na kuelewa kwenye soko lazima kuzibitiwe ili wanunuzi wasinunue kwa lumbesa na wao kama halmashauri wanasisimamia kwenye mageti yao wanapotoza ushuru kabla ya sheria mpya watahakikisha mwenye lumbesa lazima ashushe apunguze kabla ya kuingiza sokoni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni