Jumatano, 28 Juni 2017

HALMASHAURI YA WILAYA KILOLO YADHAMILIA KUMALIZA KATIKA SEKTA YA AFYA KWA KUJENGA HOSPITALI YA KISASA

Baadhi ya Majengo ya Hospitali ya Kisasa ya Halmashauri ya wilaya ya Kilolo
Halmashauri ya wilaya kilolo imedhamilia kumaliza kero inazowakabili wananchi hususani katika sekta ya afya kutokana na mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya wilaya itakayowahudumia zaidi ya  kata 12 za wilaya hiyo kutokana na kuikosa huduma hiyo kwa muda mrefu na kulazimika kuitafuta katika hospital ya Rufaa ya mkoa wa Iringa

Aloyce Kwezi ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilolo Aloisi Kwezi na Asiah Abdallah ni mkuu wa wilaya hiyo waliiambia SAYARI YA HABARI kuwa  halmashaurii hiyo inaendelea na ujenzi wa Hospitali ya kisasa ya wilaya kwa kushirikliana na wakala wa Majengo nchini TBA ikiwa ni miongoni mwa miradi itakayo kuwa na Tija ya moja kwa moja kwa wanachi kutokana na adha waliyoipata ambapo ujenzi huo unatarajia kukamilika kwa muda wa miezi 8 kwa mujibu wa mkataba wa ujenzi ambapo mpaka hivi sasa imesalia miezi miezi 2 kumalizika kwa muda uliotengwa ili wananchi kuanza kuifurahia halmashauri yao.

Viongozi hao wa Halmashauri ya wilaya kilolo walisema kutokana na Jografia ya wilaya hiyo changamoto kubwa ni namna wananchi wanavyoweza kupata huduma za afya hususani wakazi wa vijiji vya Kiwalamo na Ruaha Mbuyuni ambapo walikuwa wanalazimika kutembea umbali mrefu kuitafuta huduma hiyo huku baadhi ya wananchi wakipoteza ndugu zao wakiwa njiani kufuata huduma za afya ambapo hivi karibuni itabaki historia.

“hapo awali wananchi wa kilolo wamepata shida sana pale wanapopata maradhi hasa wanawake wajawazito waliokuwa wanahitaji huduma ya dharura(upasuaji)kwa kuwa katika Halmashauri yetu hatukuwa na hospitali kubwa walilazimika kwenda Iringa mjini katika hospitali ya Rufaa au kwenda katika hospitali Teule ya Ilula jambo lililosababisha baadhi ya akina mama na watoto kupoteza maisha wakiwa njiani tulikuwa hatuna namna”.walisema viongozi hao

“wanaendelea kusema kwasasa tunao mradi mkubwa wa ujenzi wa hospitali unaogharimu kiasi cha shilingi billion 4.2 hii itakuwa hospitali ya mfano kwani tunamajengo matano ya Ghorofa moja moja yanaendelea kujengwa hisa sasa yanakaribia kuanza shughuli za upauaji na kufikia mwezi wa nane tunaweza kuwa katika hatua ya umaliziaji na wananchi wataanza kufurahia upatikanaji wa huduma za afya na itasaidia sana kupunguza foleni katika hospitali za Rufaa na Hospitali ya Manispaa ya iringa.”walisema

Akizungumzia ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wa miradi hiyo mwenyekiti wa Halimashauri ya wilaya kilolo Valensi Kihwaga alisema Halmashauri imeendelea na uelimishaji wa wananchi katika kutambua umuhimu wa miradi iliyopo ili waweze kuisimamia na kiutumia ipasavyo huku akiwataka waendelee kuonesha ushirikiano kwa serikali katika kutekeleza miradi hiyo.

“mimi nisema tu Halmashauri yetu imedhamiria kumaliza kero za wananchi kwa kiasi kikubwa na hasa kwa kuwashirikisha wananchi wenyewe na tumeendelea kutoa elimu ya kutosha kwao ili wao ndiyo wawe wamiliki wa miradi ya maendeleo hasa hii Hospitali kubwa ambayo tunaijenga kama serikali tutahakikisha tunasimamia na kukamilisha kwa wakati ujenzi wake na ianze kutoa huduma”alisema kihwaga

Halmashauri ya Kilolo kwa ujumla imekusudia kupunguza kero za huduma za Jamii kwa wananchi ikiwemo miradi ya barabara,Maji na Elimu ili kufanya wilaya hiyo ikue kiuchumi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni