Jumapili, 25 Juni 2017

IBADA YA KUMUINGIZA KAZINI ASKOFU MTEULE BLASTON GAVILE DAYOSISI YA IRINGA



 Waumini wa kanisa la kiinjili Tanzania KKKT Dayosisi ya Iringa wameungana pamoja katika viwanja vya Shule ya msingi Gangilonga kumpokea Askofu Mpya wa Kanisa hilo Mch Blaston Gavile ili kuanza kuongoza Rasmi kanisa hilo huku Ibada hiyo ikiongozwa na Mkuu wa Kanisa KKKT  Askofu Dkt Frederick Shoo pamoja na askofu mstaafu Dkt Owdenburg Mdegella.

Askofu Mteule Gavile anachukua mikoba inachwa na Askofu Owdenburg Mdegella aliyeongoza Dayosisi hiyo kwa zaidi ya miaka 30 ambapo Askofu Mdegela katika kipindi cha uongozi wake amefanikisha kuanzisha miradi mbalimbali ili kulifanya kanisa hilo liweze kujiendesha lenyewe pasipo kutegemea ufadhiri hii inatajwa kuwa ni miongoni mwa mafanikio makubwa aliyoyapata katika uongozi wake huku waumini wa kanisa hilo wakisubiri kuona mabadiliko makubwa zaidi kutoka kwa Mch Gavile.


Endelea kutufuatilia tukujuze kila kinachojili.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni