Jumamosi, 13 Septemba 2014

USIKATE TAMAA MPENDWA NAFASI YAKO BADO IPO



HATUA ZA KUPAMBANA NA CHANGAMOTO ZA MAISHA


Katika Maisha tunapitia mambo mengi sana ambayo kwa  namna moja au nyingine hufanya maisha kuvutia au sometimes
kukarahisha, Hii ni hali ya kawaida kwa Binadamu hivyo basi yabidi kukubaliana nayo coz hizo ni just 'ups' n 'downs' katika maisha ila chamsingi ni kutokata tamaa na daima kusonga mbele.
Kero za maisha (stress) husababishwa na mambo mengi sana ikiwemo Ugumu wa maisha,kazi, mapenzi,Familia,Masomo n.k
Baadhi ya MAMBO MUHIMU yanayoweza kukuongoza kupambana na hizi kero za maisha(stress) ni kama zifuatavyo-:
1. UGUMU WA MAISHA Hili ni tatizo kubwa Dunianikotehivyo basi haina haja ya kujipa stress kama maisha
yamekua magumu kwako basi ndiyo mwisho wa kila kitu cha msingi ni kuweza kumiliki ulivyonavyo kinachotutesa wengi
wetu ni kutaka mambo makubwa wakati uwezo ni mdogo.
Yanini ukakope ili kuweka heshima mtaani au kujifanya
unakula burger daily wkt kipato chako ni cha chini? kua simplefanya vitu vya uwezo wako hapo daima utaenjoy chamsingi ni kua na malengo ya maisha yako si vyema kuishi
maisha kwa kuiga wengine mana hujui njia walizopitia. Pia ni muhimu kuweka akiba kwa ajili ya mabadiliko yoyote katika maisha kumbuka leo unafanya kazi au unapata pesa lakini ipo siku unaweza ukafukuzwa kazi au hutopewa tena pesa so yabidi kujiandaa kwa kipindi kama hicho. Remember SelfCommitment is what matters in everything you do.
2. KAZI Kazi halali humfanya mtu kua na amani moyoni hatakwa mwenyezi Mungu hivyo ni muhimu kufanya kazi kwa bidii.
Kazi pia humfanya mtu kuheshimika machoni pa wengine hata kama ukipatacho ni kidogo. Ikumbukwe kuna watu wengi sana wako mitaani wakitafuta kazi hivyo ni muhimu kumshukuru Mungu kama wewe ni kati ya wateule wake. Ukiwa kazini
mambo mengi hutokea kama kukwaruzana na Bosiauwafanyakazi wengine lkn hiyo haipaswi kukunyima rahaau kukukatisha tamaa kwani daima binadamu hatuko sawa na hiyo ilishawahi kuwatokea watu wengi sana duniani so
usijione kama 'jumba bovu limekuangukia'.
Ukiwa katika foleni tazama nje utakuta ombaomba wengi haohawakupenda kua ombaomba wala hawakuzaliwa hivyo so tutunze kazi zetu na kuzipenda pia.  kwa wale ambao bado wanatafuta kazi msikate tamaa yaweza kupita muda mrefu
usipate kazi hiyo yaweza kua ni somo ambalo umepewa ili utakapopata kazi uweze kuithamini, chamsingi ni kusali na
kumwomba Mungu katika yote uyapitiayo. Remember PRAYER is an essential element in human survival.
3.MAPENZI "Mapenzi yana run dunia" ni kati ya misemo maarufu duniani kuhusu mapenzi. Kiukweli uchaguzi wa nani uwe nae ni muhimu sana katika kukuondolea stress
maishani trust me kama ukichemka hapa ndo umechemka maishani na utabaki na stress milele so what should you do? Kwanza ni kujitahidi kua na mpenzi mmoja ambae moyo wako umeridhia kua nae mtu ambae ukiwa nae unajickia faraja,mtu ambae mnaendana kifikra na kiimani ikumbukwe " Love is the spiritual relationship" so spiritually muwe mnaendana kwani kwa kufanya hivyo itapunguza stress ktk maisha mana
hakutakua na kupingana katika maamuzi ya nini kifanyike muda gani.
Stress nyingi huletwa na watu kua na wapenzi wengi na kudhani kama wanapata 'Total satisfaction' huko ni kujidanganya hakuna jipya unalolipata kwa kua na wapenzi tofauti tofauti zaidi yamagonjwanakuzidishastress.'Kamahuridhishwinaunachokipata zungumza na umpendae ukupatie ili maisha yaendelee'.
Pia ni muhimu kutokua na rush katika swala la ndoa kwani ni muhimu sio kukimbilia kuoa bali ni kua na uhakika na huyo unaempa maisha yako awe mwenza wako. Muhimu pia kumshirikisha Mungu katika uchaguzi wako wa nani uwe nae kwani mume au mke mwema anatoka kwa Mungu.

4.FAMILIA Familia ni kiungo muhimu kinachoweza
kukuongezea au kukupunguzia stress hivyo basi familia inabidi ichukuliwe kwa makini sana. Familia yatakiwa iwepo kukusuport na kukushauri lakini usikubali familia kukuharibia mipango na malengo yako. Ni vizuri kusaidia mambo ya kifamilia lakini kamwe usiruhusu mambo hayo yachukue kila furaha uliyonayo maishani. Yani kama unao uwezo wa kusaidia ni vizuri ukasaidia itakupa baraka kwa Mungu na kwa yule umsaidiae. Lkn kamwe msaada usizidi uwezo.Ikiwezekana hata
waweza kuwapotezea wanafamilia in the process of making good life mana mwisho wa yote utabaki wewe kama mama/baba
wa familia na hao wengine watakua na familia zao. Vivyo hivyo hata kwa marafiki pia kama unaona hawakusaidii lolote let them go.
5.MASOMO Kusoma kwa bidii na kuzingatia kinachokufanya usome ni njia nzuri ya kuepukana na stress zinazosababishwa na
kufail mitihani au kupanic wakat mitihani ikikaribia.
Hakuna uchawi katika masomo ni kwamba tunatakiwa tukuweka fikra zetu na muda wetu kusoma mambo mengi ili kuepukana na stress za sup na failures ktk masomo. Najua kuna mambo mengi ambayo ukiyafanya waweza kua stess free man/
woman chamsingi ni
KUTHAMINI ZAIDI MAISHA YAKO NA KUYACHULIA KAMA NDO KILA KTU KWAKO. Ukitaka chukua ukiona haikusaidii achana nayo mana hizi sio fomula.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni