Jumatano, 24 Septemba 2014



 MH.MGIMWA AWAHAMASISHA VIJANA KUUNDA VIKUNDI ILI WAWEZESHWE.
Mh.Gogfrey Mgimwa Mbunge wa Jimbo la Kalenga
Vijana nchini wametakiwa kujiunga katika vikundi vya ujasiliamali vitakavyo warahisishia kupewa dhamana ya mitaji kutoka katika mifuko ya vijana ya serikali.

Rai hiyo imetolewa na Mbunge wa Jimbo la Kalenga mkoani hapa Mh.Godfrey Mgimwa wakati wa mahojiano maalumu na Overcomers redio katika kipindi cha tujadili asubuhi kuhusu namna viongozi wanakusudia kuwapa fulsa vijana wote pasipo kuangalia mjini wala vijijini.

Mh.Mgimwa amesema imefika wakati wao kama viongozi vijana kupigania maslahi ya vijana na haki zao za kuwezeshwa kimaisha ili waweze kujikwamua kiuchumi kwani kwa kufanya hivyo fedha za mifuko ya vijana zitawafikia katika vikundi.

Hivyo amewataka vijana kushirikiana kwa pamoja katika kujiletea maendeleo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni