MH.MGIMWA AWAHAMASISHA VIJANA KUUNDA VIKUNDI ILI WAWEZESHWE.
Vijana nchini wametakiwa kujiunga katika vikundi vya
ujasiliamali vitakavyo warahisishia kupewa dhamana ya mitaji kutoka katika
mifuko ya vijana ya serikali.
Rai hiyo imetolewa na Mbunge wa Jimbo la Kalenga
mkoani hapa Mh.Godfrey Mgimwa wakati wa mahojiano maalumu na Overcomers redio
katika kipindi cha tujadili asubuhi kuhusu namna viongozi wanakusudia kuwapa
fulsa vijana wote pasipo kuangalia mjini wala vijijini.
Mh.Mgimwa amesema imefika wakati wao kama viongozi
vijana kupigania maslahi ya vijana na haki zao za kuwezeshwa kimaisha ili
waweze kujikwamua kiuchumi kwani kwa kufanya hivyo fedha za mifuko ya vijana
zitawafikia katika vikundi.
Hivyo amewataka vijana kushirikiana kwa pamoja
katika kujiletea maendeleo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni