Jumatatu, 3 Julai 2017

UJERUMANI MABINGWA KOMBE LA MABARA 1-0 DHIDI YA CHILE

media
Michuano ya kombe la Mabara imemalizika na Hatimaye Timu ya Soka ya Taifa ya Ujerumani imeibuka Bingwa mara baada ya kumtandika bao Moja kwa Sufuli timu ya Taifa ya Chile ambaye katika mchezo wao uliopita Chile vs Ujerumani walitoka sare ya bao moja kwa moja uliochezwa kwenye uwanja wa Kazan Arena huko Kazan, Urusi.

Jumapili usiku, Julai 2, kumefanyika mtanange wa mechi moja ya fainali, ambapo timu ya taifa ya Ujerumani ambao ni mabingwa wa kombe la dunia lililopita nchini Brazil ambapo kwa sasa chini ya Mwalimu Joachim Löw ambaye amekiandaa kikosi cha Ujerumani na kurudisha heshimaya Soka nchini Ujerumani.

Ujerumani iliingia uwanjani kwenye mchezo huo, ikiwa na historia nzuri ya kuanza vyema michuano ya mwaka huu mpaka kwenye hatua waliyofikia baada ya kutopoteza mchezo hata mmoja.

Ujerumani imetengeneza Historia ya kuwa timu nyingine itakayofanikiwa kutwaa taji la michuano ya Ulaya baada ya lile la kombe la dunia kama ilivyowahi kufanya timu ya taifa ya Hispania, iliyotwaa kombe la dunia mwaka 2010 na kushinda taji la Ulaya mwaka 2012.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni