Jumapili, 2 Julai 2017

TAIFA STARS YASONGA NUSU FAINALI BAADA YA KUTOA DOZI YA GOLI 1-0 DHIDI YA AFRIKA KUSINI


Image result for kikosi cha taifa stars 2017
Timu ya Soka ya Tanzania Taifa Stars imeibuka na ushindi wa goli 1-0 thidi ya Afrika Kusini katika michuano ya Balaza la Soka katika nchi za kusini Mwa Africa COSAFA ambapo katika dk 18 mchezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania Elius Mguli jezi nambali 12 mgongoni aliwainua mashabiki kwa kupachika Bao la kwanza na la Ushindi.
Taifa Stars ilifuzu kuingia katika hatua ya robo fainali ya mashindano ya michuano ya COSAFA inayo endelea huko nchini Afrika Kusini baada ya kutoka sare ya goli moja kwa moja dhidi ya Mauritius.
Huko Afrika kusini Timu yua Tanzania ikicheza na Wenyeji wa Mashindano hayo Afrika Kusini imekuwa ilicheza mchezo wa kuvutia kuonesha ukomavu wa soka huku timu ya wenyeji wakidharu mchezo huo ambapo imewagharimu na sasa watabaki kuwa watazamaji wa wa Mashindano hayo baada ya kutolewa kwa Goli moja kwa sufuli.
Akizungumza mara baada ya mchezo huo Mcheza Mhimu katika mchezo huo(MAN OF THE MARCH)Elius Maguli amesema walipata nafasi na wameitumia na kupata goal lililowapeleka kwenye Nusu Fainali
“tunashukuru tumetumia nafasi tuliyoipata tumeshinda cha msingi ni kujiandaa katika michezo mingine”alisema mchezaji huyo
Katika michuano hiyo Taifa Stars imekuwa ikionesha tofauti na Timu zingine kwani Hadi leo imepata nafasi ya kutoa Man Of The March kwa mara ya Nne mfurulizo
Sayari ya Habari inaitakia Taifa Stars Ushindi katika mechi zijazo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni