MUCOBA BENKI YAWA CHACHU YA MAENDELEO KWA WAKULIMA MKOANI
IRINGA
| Meneja wa Benki ya Wananchi MUCOBA Bw Beny Mahenge akielezea utendaji wa Benki hiyo |
| Wadau wa Benki ya wananchi MUCOBA |
Wakulima wa mkoa wa Iringa wameanza kunufaika na ruzuku za
pembejeo kupitia Benki ya wananchi Mufindi(MUCOBA) ambayo kwa sasa inajulikana
kwa jina la MUCOBA Bank PLC ikijumuisha wananchi wote wa mkoani wa Iringa imeanza
kutoa mikopo ya pembejeo kwa vikudi vya wakulima.
Akielezea juu ya namna mwananchi atakavyonufaika na ruzuku
hiyo Meneja wa Benki hiyo Bw Ben Mahenge amesema serikali imeamua kutoa ruzuku
kwa mkulima kupitia Benki ya wananchi kutokana na ukaribu wa Benki hiyo kwa
wananchi wa maeneo yote ya mkoa wa Iringa ili kulinda usalama wa chakula kwa
mkulima.
Amesema kuwa walengwa wakuu ni wananchi wa kipato cha chini
ili wawe na uhakika wa kupata chakula cha kutosha hususani kwa wale waliolima
ukubwa wa shamba la kuanzia ekali moja ambao watasaidiwa kupatiwa ruzuku ya
mifuko mitatu ya mbolea na mfuko mmoja wa mbegu kwa mazao ya Mpunga na Mahindi
ikiwa ndiyo mazao pekee yanayopendelewa na wananchi wa mkoa wa Iringa.
Bw Mahenge ameendelea kufafanua juu ya ruzuku hizo kuwa
itatolewa kwa wakulima watakaojiunga katika vikundi mbalimbali
vitakavyojumuisha wanakikundi wasiopungua 10 ambao kila mmoja atapatiwa mkopo
wa pembejeo zenye ruzuku ya serikali.
Ameelezea kuwa ruzuku hiyo itatokana na riba ya mkopo
atakaoupa kutoka benki ambayo ghalama yake ya ni 18% ambapo serikali inalipa
riba ya asilimia 14% ya riba ikiwa kwa upande wa mkulima atalipa riba ya
asilimia 4% kutoka kwenye riba ya asilimia 18% ya mkopo wote.
Aidha amesema kupitia benki hiyo ya MUCOBA wananchi
watajipatia pembejeo wanazozihitaji badala ya kupangiwa aina ya pembejeo za
kilimo ili kuboresha zaidi kipato na mazao ya mkulima ambapo amesema mkopo huo
utalipwa baada ya mavuno pamoja na kwa kabla ya mkulima kupewa mkopo huo
atatakiwa kulipa asilimia 20 ya kianzio kuonesha nia ya kuhitaji ruzuku.
Hivyo amewataka wananchi kushiriki katika vikundi mbalimbali
ili wawe sehemu rahisi ya kupata pembejeo zenye ruzuku ya serikali kwa urahisi
zaidi pia amewataka wakulima kumchangua wakala wa pembejeo atakayeshirikiana
katika kuzipata zenye viwango vya hali ya juu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni