MADIWANI MANISPAA YA IRINGA WAANZA KUTAKELEZA KAULI YA
KATIBU MKUU WA CCM KWA VITENDO.
Baraza la Madiwani manispaa ya Iringa lakumbushwa umuhim wao
katika kusimamia miradi ya Maendeleo ikiwa ni nguzo ya muhim katika kuendeleza
uchumi wa familia,jamii na Taifa.
Hayo yamejili mwisho wa wiki katika kikao charobo ya mwaka
wa fedha 2014/2015 cha Baraza la
Madiwani wa halmashauri ya Manispaa ya Iringa mjini ambapo Meya ambaye pia
ndiye alikuwa mwenyekiti wa baraza hilo Aman Mwamwindi aliwambia madiwani kuwa
nisehemu ya serikali hivyo wanaowajibu wa kusimamia miradi inayoanzishwa na
serikali ikiwemo miradi ya Afya,elimu,miundombinu na shughuli za uchumi ili
kuongeza upatikanaji na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Alisema pamoja na kwamba madiwani hao wanashiriki kwa kiasi
kikubwa katika usimamizi wa miradi hiyo lakini pia alipata fulsa ya
kuwakumbusha kuwa usimamizi wa miradi hiyo unashirikisha viongozi wa ngazi ya
kijiji hadi Taifa,wananchi wa maeneo husika pamoja na asasi za kiraia na
kashirika yasiyo ya kiserikali ikiwa na lengo la kuboresha maisha ya watanzani.
“Waheshimiwa madiwani
tumekuwa mstari wa mbele kusimamia miradi inayoanzishwa katika kata zetu japo
wapo wachache ambao kazi yao ni kuturudisha nyuma kwa makusudi maana tumekuwa
na miradi mingi na inafanya vizuri kwaajili yetu sote na jamii zinazotuzunguka
sasa unapoona mtu anaingiza kitu ambacho kinarudisha nyuma juhudi za serikali
ukanyamaza manaake unashiriki mojakwamoja kuangamiza maisha ya
watanzani”alisema meya
Hivyo amesema usimamizi mbovu wa miradi ya maendeleo mara
nyingi inasababisha baadhi ya miradi kufanyika chini ya kiwango.
Baraza hilo pia lilipata nafasi ya kupata semina juu ya
ushiriki wao katika mapambano dhidi ya rushwa ambalo limekuwa janga la dunia
ambalo limekuwa likiwahusisha zaidi watendaji wa serikali.
Akitoa semina hiyo Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana
na Rushwa(TAKUKURU)Bw Ismail Bukuku aliwambia madiwani kuwa lengo la semina
hiyo ni kuwakumbusha uwajibikaji kwa kufuatamisingi ya sheria huku wakitambua
usimamizi mzuri wa raslimali za umma kutasaidia kuziba mianya ya
Rushwa,itasaidia fedha za miradi kutumika kwa malengo yaliyo kusudiwa.
Huku akiwataka madiwani hao kuwaelimisha wananchi kutambua
haki zao katika kupata huduma za msingi ikiwa nipamoja na matibabu,ajira,elimu
bila kutoa wala kupokea rushwa vilevile
kuzijua sheria.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni