EXAUD KIGAHE AGOMBEA NAFASI YA UBUNGE JIMBO LA MUFINDI KASKAZINI.
![]() | |
| Exaud Kigahe Mgombea Ubunge Jimbo la Mufindi Kaskazini |
Ikiwa mchakato wa kutangaza nia ya kugombea Ubunge
na Urais hapa nchini unaendelea jamii imetakiwa kuwachagua watu wenye nia ya
dhati ya kuwaletea maendeleo chanya katika maeneo husika.
Hayo yamesemwa na Mdau wa maendeleo wilayani Mufindi
Bw Exaud Kigahe wakati akizungumza na wandishi wa habari Mjini mafinga
wailayani Mufindi Mkoani Iringa wakati akitangaza nia ya kugombea nafasi ya Ubunge
katika Jimbo la Mufindi kasikazini ambapo amesema ni vyema na wakati umefika
kwa wananchi kuwachagua viongozi wenye uwezo na uzalendo wanaoweza kushirikiana
nao katika kuleta maendelaeo.
“ni ukweli usiopingika kwamba wakati wa viongozi
kuwarubuni wananchi umekwisha ninahakika kwamba Mufindi ninaijua vizuri sana
yale maisha wanayaishi wananchi wale siyo ndiyo waliyotakiwa kuishi nimekuja
kushirikiana nao tuondoe tatizo la umaskini kikubwa nikipewa ridhaa kwangu
wajibu wangu ni kuwaletea maendeleo wananchi” alisema Kigahe
Bw Kigahe amesema mtazamo wa sasa katika kusimamia
shughuli za maendeleo zinatazamwa zaidi kwa viongozi ambapo anapotokea kiongozi
ambaye hana uwezo hakuna maendeleo yatakayopatikana kwa wakati hivyo amesema
endapo atapata nafasi ya kuongoza jimbo hilo kuna mambo lukuki anayoyaona
yakitumika kama furusa kwa wananchi wa Mufindi yatawapa maendeleo kwa kasi
wananchi hao.
Amesema wilaya ya Mufindi ni miongoni mwa wilaya
zenye raslimali za kutosha ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikituwa na wageni
huku wazawa wakibaki kuwa walinzi jambo ambalo amesema kusingekuwa na maendeleo
hata kwa miaka ijayo bali kwa kutumia rasilimali hizo atahakikisha
anawaunganisha wananchi kwa ushirikishaji wa mambo yote ya maendeleo kwa faida
ya wanamufindi wenyewe.
“rasirimali zilizopo ninaamini zinatosha sana
kutuletea maendeleo wanamufindi ninachokifahamu kwa mufindi na kwamba tuna
misitu lakini kutokana na uongozi kutotujali wamekuwa wakitumia watu wa maeneo
mengine nadhani muda wa wananchi kutumia misitu yao umewadia nitafurahi nao na
kulia nao” alisema
Pia Kigahe amesema inasikitisha kuona rasirimali
kama misitu inavunwa na watu wa nje na wenyeji wakibaki maskini jambo ambalo
haliwezi kuvumilika,amesema wilaya ya Mufindi ina ardhi ya kutosha ambayo kwa
kiasi kikubwa haiwanufaishi wanamufindi.
Hivyo amewataka wananchi kwasasa wasidanganyika na
watu wanakuja wakiwa hawana malengo mema na wananchi bali wanahitaji
kujinufaisha wenyewe bali sasa amekuja kwaajili ya kushirikiana nao kuiondoa
hali hiyo.
“kwa upande
wangu ninaamini kwamba wanamufindi wanahitaji mambo makubwa machache tu ambayo
nikipata ridhaa na wakati maalumu ukifika nitawaeleza na namna tutakavyo weka
mikakati ya maendeleo mimi ninauchungu na maisha yale wanayoishi mama zetu,baba
zetu hata wadogo zetu naomba wanipokee tuyamalize hayo” ni maneno ya Kigahe
Jimbo la Mufindi Kaskazini lenye kata 11 za Ikweha, Sadani, Igombavanu, Ifwagi, Mdabulo, Ihalimba, Kibengu, Mapanda, Mpanga Tazara, Ihanu na Ikongosi, Jimbo la Mufindi Kusini litakuwa na kata 14 za Kiyowela, Makungu, Mninga, Kasanga, Igowole, Mtambula, Itandula, Mbalamaziwa, Idunda, Mlangali, Nyololo, Ihowanza, Mtwango na Luhunga:
Jimbo la Mufindi Kaskazini lenye kata 11 za Ikweha, Sadani, Igombavanu, Ifwagi, Mdabulo, Ihalimba, Kibengu, Mapanda, Mpanga Tazara, Ihanu na Ikongosi, Jimbo la Mufindi Kusini litakuwa na kata 14 za Kiyowela, Makungu, Mninga, Kasanga, Igowole, Mtambula, Itandula, Mbalamaziwa, Idunda, Mlangali, Nyololo, Ihowanza, Mtwango na Luhunga:


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni