Jumatatu, 8 Juni 2015



 UVCCM IRINGA KUSAIDIA JITIHADA ZA SERIKALI KUHAMASISHA VIJANA KUJIARI NA KUPAMBANA NA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI.
katibu wa UVCCM mkoa wa Iringa, Elisha Mwampashi wa pili kulia akiwa na katibu mkuu wa UVCCM Taifa Bw Sixtus Mapunda.
Vijana nchini hususani mkoani Iringa wameshauriwa kujiandaa na kujiweka sawa katika kupambana na changamoto za ugumu wa maisha kwa kuchangamkia furusa mbalimbali zinazojitokeza na kujiajiri wenyewe.

Kauli hiyo imekuja baada ya tafiti mbalimbali zilizofanywa na kuonesha kuwa vijana wengi wamekuwa na mitazamo ya kusubiri serikali iwaletee badala ya kufikiri zaidi namna ya kujitengenezea ajira zitakazo waletea kipato na kuboresha maisha yao hali ambayo imeendelea kuwarudisha nyuma kimaendeleo.

Akitoa tathimini ya kikao  cha Baraza la vijana mkoa wa Iringa Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Bw Elisha Mwampashe amewataka vijana wafanye kazi ili wasiendelee kuilamu serikali.

“ninawaomba vijana ifike wakati tujitambue na tuone jukumu la kujiletea maendeleo katika familia zetu tusiwe watu wa kulaumu tu badala kuwa na mawazo chanya kujishughulisha na shughuli zitakazotuletea maendeleo ili hata kama kuna mkono wa serikali kusaidia jitihada zetu utukute tukiwa tayari tuna mambo tunafanya” alisema mwampashe

Aidha  alisema maadhimio ya vijana wa chama cha mapinduzi  katika kikao hicho ni kutoa elimu kwa vijana itakayowasaidia kutumia changamoto zilizopo kuwa fulsa zitakazo waingizia kipato pia ameeleza maadhimio mengine kuwa ni kuwatembelea vijana na kubaini changamoto zinazowakabili na kutafuta namna ya kuzimaliza mengine ni kusaidia katika shughuli za kijamii ambapo mapema mwezi huu wanatarajia kuweka kambi ya pamoja kwaajili ya kufyatua tofari na kuanza ujenzi wa Bweni la shule ya sekondari Idodi lililoteketea kwa moto hivi karibuni kama vijana wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa iringa ili kupunguza nguvu ya wananchi katika kuchangia ujenzi huo.

“tumefanya kikao cha baraza la vijana wa Chama Cha Mapinduzi na tumejadili na kuadhimia mambo mengi ambayo tunaamini tutayasimamia na kuyatekereza kama vijana tumeadhimia kuwafikia vijana wengi ili kuangaliachangamoto zinazowakabili na tuone namna ya kuzitatua na vijana wenyewe kuhakikisha tunatengeneza vikundi vya kiujasiliamali vitakavyotuwezesha kupata wafadhiri”.alisema

Hivyo Mwampashe amesema wao kama vijana watahakikisha wanawafikia vijana wote wa mkoa wa iringa ili kukumbushana wajibu wao katika kujiletea maendeleo na kutambua kuwa vijana ndiyo nguvu kazi ya Taifa.

Mwampashe amesema sio jambo jema kwa vijana wenye nguvu kushinda vijiweni wakizungumza siasa na kucheza bao wakati wenzao wakiwa katika shughuli zao mbalimbali za kiuchumi.

“tumepita katika vikundi kadhaa hapa mkoani na tayari tumekutana na baadhi ya vijana wanaojishughulisha na ujasiliamali tumezungumza nao tumewapa elimu na baadhi ya vitendea kazi kama mashine ya ufyatuaji tofari na kuwahamasisha umoja kwa mustakabari wa maisha yao kwa kuwa kumekuwa na kasumba ya vijana wanaokaa vijiweni bila kazi yoyote na kuilamu serikali  jambo ambalo halina manufaa yoyote kwao”.alisema mwampashe katibu wa vijana

Alisema duniani kote hakuna serikali inayoweza kuajiri kila mtu mwenye uwezo na sifa za kufanya kazi na akazungumzia umuhimu wa sekta binafsi katika kushughulikia changamoto ya ajira kwa vijana.

Akizungumzia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka hu, Mwampashe amewataka wanawake kuondoa hofu na kujitokeza kwa wingi kushindana na wanaume katika nafasi mbalimbali za uongozi zinazogombewa.

Pamoja na wanawake, amewasishi vijana wenye sifa kutupa karata zao katika uchaguzi huo huku akiwataka wajiandikishe kwa wingi na kushiriki kikamilifu kuchagua viongozi bora wanaojali matatizo yao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni