Jumatatu, 25 Mei 2015

CAROLINE ACHERY MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJIRI MWENYE MALENGO NA MTAZAMO WA MBELE KATIKA HUDUMA NA KATIKA JAMII

Caroline katika Ubora wake
Ni mwimbaji wa nyimbo za Injiri jijini Dar es salam ambaye amekuwa na malengo ya kufika mbali pia kupitia huduma yake ya Uimbaji amepanga malengo makubwa ya kuisaidia jamii
"mimi katika huduma ya uimbaji nilianza kitambo kidogo toka nikiwa mtoto nilikuwa naimba Sunday School nimekuwa hivo nikaingia katika kwaya ambako hadi sasa ni kiongozi wa Kuabudu kanisani na mshukuru Mungu ananitumia katika kuabudu na nitaendelea kumuabu siku zote" alisema Caroline

Ni miongoni mwa waimbaji wachache ambao tayari pamoja na shughuli zao binafsi amefanikiwa kuwa na kituo kidogo cha kulea watoto yatima kilichopo mkoani Arusha akiwa na malengo ya kuwa mlezi wa watoto yatima na Wajane  kituo hicho kipo Umasaini huko na Kinafahamika kwa Jina la LOBOSIRETI naamini kwa wakazi wa Arusha wanalijua maana ya jina hilo. ''mimi napenda kwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu hivyo namshukuru Mungu nimefanikiwa kuanzisha kituo cha watoto yatima na wajane ambacho kimsingi bado kichanga kutokana na uhaba wa fedha za kukiendesha bali namwamini mungu atanipa kwasababu nimaombi yangu kituo kile kifanikiwe kiwe msaada wawatu wasiojiweza" alisema

Pia kuhusu kutoa albamu zake za nyimbo alisema yeye amefanikiwa kuwa na albam Moja haya ni maneno yake"albam yangu ya kwanza Inaitwa 'MWANGALIE MUNGU' niliitoa mwaka 2008 na kuiweka wakfu mwaka 2009 katika kanisa la maranatha Arusha ambako ndiko ninakolelewa kiroho toka nina umri wa miaka nne mpaka leo" alisema


Akizungumzia Ujio wa Albam yake mpya ya Audio Caroline amesema anatajia kuitoa siyo muda mrefu kuanzia sasa na kuwataka mashabiki wake wa muziki wa Injiri kukaa mkao wa Burudani kwani itakuwa ya Viwango hivyo wamsapot kwa mawazo hata kwa kuitafuta kwani anasema"namshukuru mungu ameniwezesha baada ya ile albamu yangu ya kwanza sasa natarajia kuitoa albamu ya pili ambayo itatoka mwezi wa sita na inatwa 'SUBIRI WAKATI WA BWANA' na ninaamini itawabariki sana" alisema hayo katika Hot Interview tuliyoifanya na mwimbaji huyu

Pia alizungumzia mpango wake wa kuzifanya albamu zake za sauti kuwa katika mfumo wa Picha anasema hiyo ni hatua ambayo anaiendea kwa sasa kwa hiyo anatarajia kuzirekodi nyimbo hizo kwa mfumo wa Video hivi karibuni " Mpango wangu ninatarajia kuja kufanya video ya Live yenye nyimbo za kuabudu na pia kutengeneza  kundi la wamwabuduo halisi ambalo litakuwa likifanya uimbaji wa Live ndani na Nje ya nchi kwa nyimbo za kuabudu na kusifu"alisema Caro

Moja kati ya mambo ya kujifunza kwa Caroline ni pamoja na kuwa na malengo pamoja na kujituma kwa mwimbaji itakuwa sehemu ya kukutoa mahali ulipo kwenda katika hatua nyingine maana unaweza kuwa ni mwimbaji mzuri kama hutakuwa na malengo katika uimbaji wako wala bidii hakika kuzifikia ndoto ni vigumu. Tunakutakia safari njema katika huduma na malengo uliyo jiwekea

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni