Jumanne, 26 Mei 2015

Unaweza kuwasiliana na Mwimbaji kwa 0757 322 501 kwa mialiko mbalimbali



JE UNAMJUA MICHAEL KOMBA? MWIMBAJI NA MUHUBIRI WA INJIRI TANZANIA?


Moja kati ya Majukumu niliyonayo ni kuhakikisha unapata habari za waimbaji wa Nyimbo za Injiri Tanzania kupita mtandao na OVERCOMERS FM 98.6 IRINGA.
 
Mtumishi wa Mungu Michael Komba akiwa katika huduma ya Maombezi katika ibada
Mtumishi wa Mungu Michael Komba akiwa katika Mkutano wa Nje.

Waimbaji waliotikisa katika Mkutano huo wa Mtumishi Komba
Mtumishi wa Mungu Michael Komba akiwa na Mkewe (TUPONILE KOMBA)
 Leo napenda uweze kumfahamu Michael Komba Mwimbaji wa nyimbo za Injiri na Muhubiri wa neno la Mungu huyu ni miongoni mwa waimbaji wanaoendelea kufanikiwa kupitia utumishi wa mungu ambapo Mungu amekuwa akimtumia kwa namna ya kipekee nay a tofauti ambapo amekuwa akitumika katika maeneo mengi ya ndani na nje ya nchi kwa njia ya uimbaji na Kuhubiri Neno la Mungu katika mikutano mbalimbali.

Tukataka kufahamu historia ya uimbaji wake Komba anasema anamshukuru Mungu kwa Neema aliyompa hadi alipofikia kwani ameanza kitambo uimbaji wake tangu akiwa mdogo mpaka kufikia alipofikia nabado anakaza moyo kusonga mbele.

“ni kweli nimeanza kitambo kweli sana mnamo mwaka 1987 baada ya kuokoka na ndipo nilipopata kibali cha kumtumikia mungu kwa njia ya uimbaji” alisema Komba

Pia hatukusita kutaka kujua komba ikiwa amfanikiwa kuwa na albamu ya nyimbo za Injiri ambayo tayari iko sokoni kwa sasa tangu alipoanza uimbaji ma mafanikio yake yakoje alisema

“nimefanikiwa kurekodi nyimbo ambazo ni albamu tangu 2009 inayofahamika kwa jina la MUNGU HALI UGALI ambayo inatamba sasa katika vituo mbalimbali vya redio hapa nchini na nje nchi na Mungu amenibariki nimeshaitengenezea video ambayo inatarajia kutoka siyo muda mrefu ambayo itakuwa yenye ubora wa kiwango cha kiutumishi hivyo mashabiki wangu na wadau wa muziki wa Injiri watarajie kitu kupitia DvD hiyo” alisema

Akizungumza namna mungu alivyo muinua katika kuhubiri neno la mungu katika mikoa mbalimbali na nje nchi komba amesema tangu mwaka 2012 amekuwa akitumika kuhubiri injiri na amemuona mungu kupitia huduma hiyo.

“Mungu amenipaka mafuta ya kunena Neno lake kwa Ufunuo usio wa kawaida mikoa mbalimbali ya Tanzania na nje ya nchi kama Jijini Nairobi Kenya na kwingineko,ninaujumbe mzito kwa kanisa naipenda sana huduma hii ninafundisha katika makongamano na semina makanisani”alisema komba

Akizungumzia Baraka ya kumpata mke wa kufanana naye komba amesema anamshukuru mungu kwaajili ya mke wake kwani amekuwa Baraka kubwa kwake kutokana na namna alivyowainua katika huduma hii alisema

“naimba na kuhubiri pamoja na mke wangu Tuponile Komba Bwana anatutumia kwa namna ya kipekee nimemuona Mungu kupitia mke wangu hususani uvumilivu wake na maombi juu ya familia yetu tuliyo nayo hii ni Baraka”alisema komba

Hivyo amesema kuwa yuko tayari kwa mialiko mbalimbali iwe uimbaji ama Kuhubiri katika mikutano mbalimbali na semina.
Unaweza kuwasiliana nae kwa Namba  0757 322 501
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni