JE UNAMJUA MICHAEL KOMBA? MWIMBAJI NA MUHUBIRI WA INJIRI TANZANIA?
Moja kati ya Majukumu niliyonayo ni kuhakikisha unapata habari
za waimbaji wa Nyimbo za Injiri Tanzania kupita mtandao na OVERCOMERS FM 98.6
IRINGA.
![]() |
Mtumishi wa Mungu Michael Komba akiwa katika huduma ya Maombezi katika ibada |
![]() |
Mtumishi wa Mungu Michael Komba akiwa katika Mkutano wa Nje. |
![]() |
Waimbaji waliotikisa katika Mkutano huo wa Mtumishi Komba |
![]() |
Mtumishi wa Mungu Michael Komba akiwa na Mkewe (TUPONILE KOMBA) |
Leo napenda uweze kumfahamu Michael Komba Mwimbaji wa nyimbo
za Injiri na Muhubiri wa neno la Mungu huyu ni miongoni mwa waimbaji
wanaoendelea kufanikiwa kupitia utumishi wa mungu ambapo Mungu amekuwa
akimtumia kwa namna ya kipekee nay a tofauti ambapo amekuwa akitumika katika
maeneo mengi ya ndani na nje ya nchi kwa njia ya uimbaji na Kuhubiri Neno la
Mungu katika mikutano mbalimbali.
Tukataka kufahamu historia ya uimbaji wake Komba anasema
anamshukuru Mungu kwa Neema aliyompa hadi alipofikia kwani ameanza kitambo
uimbaji wake tangu akiwa mdogo mpaka kufikia alipofikia nabado anakaza moyo
kusonga mbele.
“ni kweli nimeanza
kitambo kweli sana mnamo mwaka 1987 baada ya kuokoka na ndipo nilipopata kibali
cha kumtumikia mungu kwa njia ya uimbaji” alisema Komba
Pia hatukusita kutaka kujua komba ikiwa amfanikiwa kuwa na
albamu ya nyimbo za Injiri ambayo tayari iko sokoni kwa sasa tangu alipoanza
uimbaji ma mafanikio yake yakoje alisema
“nimefanikiwa kurekodi
nyimbo ambazo ni albamu tangu 2009 inayofahamika kwa jina la MUNGU HALI UGALI ambayo
inatamba sasa katika vituo mbalimbali vya redio hapa nchini na nje nchi na
Mungu amenibariki nimeshaitengenezea video ambayo inatarajia kutoka siyo muda
mrefu ambayo itakuwa yenye ubora wa kiwango cha kiutumishi hivyo mashabiki
wangu na wadau wa muziki wa Injiri watarajie kitu kupitia DvD hiyo” alisema
Akizungumza namna mungu alivyo muinua katika kuhubiri neno
la mungu katika mikoa mbalimbali na nje nchi komba amesema tangu mwaka 2012
amekuwa akitumika kuhubiri injiri na amemuona mungu kupitia huduma hiyo.
“Mungu amenipaka
mafuta ya kunena Neno lake kwa Ufunuo usio wa kawaida mikoa mbalimbali ya
Tanzania na nje ya nchi kama Jijini Nairobi Kenya na kwingineko,ninaujumbe
mzito kwa kanisa naipenda sana huduma hii ninafundisha katika makongamano na
semina makanisani”alisema komba
Akizungumzia Baraka ya kumpata mke wa kufanana naye komba
amesema anamshukuru mungu kwaajili ya mke wake kwani amekuwa Baraka kubwa kwake
kutokana na namna alivyowainua katika huduma hii alisema
“naimba na kuhubiri pamoja na mke wangu Tuponile Komba Bwana
anatutumia kwa namna ya kipekee nimemuona Mungu kupitia mke wangu hususani
uvumilivu wake na maombi juu ya familia yetu tuliyo nayo hii ni Baraka”alisema
komba
Hivyo amesema kuwa yuko tayari kwa mialiko mbalimbali iwe uimbaji ama Kuhubiri katika mikutano mbalimbali na semina.
Unaweza kuwasiliana nae kwa Namba 0757 322 501