Jumatano, 18 Februari 2015



TASAF KUWANUFAISHA WANAOISHI MAZINGIRA MAGUMU
 
NA AGUSTINO KIHOMBO IRINGA

Zaidi ya kaya elfu sita zinazoishi katika mazingira magumu za manispaa ya Iringa zinatarajia kunufaika na mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF katika awamu ya tatu ya mpango wa kupunguza umasikini kwa jamii.

Akizungumza na mtanandao huu Mratibu wa Mfuko huo Manispaa ya Iringa Bi Lucy Mtafya alisema kuwa mpango wa matumizi ya mufuko huo umegawanyika katika awamu tatu ambapo katika awmu ya Kwanza mfiko huo wa maendeleo ulijikita zaidi katika kusaidi katika uboreshaji wa huduma za Elimu na Afya hususani ujenzi wa shule na Zahanati.

Akielezea juu ya Awamu ya kwanza ya TASAF alisema wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kusaidia shughuli za maendeleo ambapo mfuko huo ulikuwa ukichangia kwa asilimia 80% ya ujenzi na wananchi 20% hivyo hadi awamu hizo mbili zimesaidi kujenga zaidi ya Shule tano na zahanati Tatu katika manisipaa ya Iringa.
“Kwa ujumla Mfuko huu wa Maendeleo ya jamii TASAF tumefanikiwa vizuri sana kuwasaidia wananchi katika shughuli zao za maendeleo mfuko huu kila mahali ulipofanya kazi ulichangia aslimia 80% na wananchi walichangia asilimia zinazo baki hiyo katika awamu hizo mbili” alisema

Akizungumzia kuhusiana na awamu hii ya Tatu ambayo imezinduliwa rasmi  Jan 6 2015 Bi Mtafya alisema tayari wamekwisha anza kushughulikia masuala ya kuzitambua kaya za watu wasio jiweza ambao ndiyo wanaolengwa na awamu hii ambapo wanalenga kuzifikia kaya zaidi ya 6000 ili kuwawezesha kiuchumi.

Mratibu huyo alisema wamejipanga kuhakikisha wanaolengwa na Mfuko huo kwa awamu hii ya tatu wananufaika na fedha zitakazotolewa na mfuko huo alisema katika manispaa wanafanya kazi na kata zote za manispaa ya iringa.
“katika awamu hii ya tatu ya Mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF imelenga kuwafikia wote wanaohusika hasa wale ambao mitaa yao itakubaliana kuwa ndiyo watakao nufaika zaidi kwani katika siku za nyuma baadhi ya watu walikuwa wanajaribu kutumia ujanja kuwandika watoto wao wasaidiwe na kuwfanya walengwa wakose” alisema

Hivyo amewataka wananchi kusaidiana na serikali katika kuwasaidia waishio katika mazingira magumu ili kuwawezesha kumudu maisha pindi awamu hiyo itakapopita.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni